Mhubiri moja nchini Nigeria ambaye amekuwa kwa ndoa kwa zaidi ya miaka 22 bila ya kupata mtoto anasherehekea kwa sasa baada ya Mungu kuyajibu maombi yake
Nnaghe Itam na mkewe sasa wamekuwa gumzo kwenye mitandao ya kijamii baada ya kujaliwa mtoto wao wa kwanza miaka 22 wakiwa na subira kwenye ndoa.
Wanandoa hao ambao wanaongoza kanisa la Faith Church (Salem Church) mjini Calabar, walijawa na kufuraha tele na kutangaza habari hizo njema kwa waumini wa kanisa hilo ambao pia walieneza ujumbe huo mitandaoni.
Mtoto huo alifikishwa kanisani ambapo aliombewa na wahubiri wengine ambao walimbariki na kumtakia maisha marefu.
Pasta aliwahimiza wale wanandoa ambao wanawatafuta watoto kutokataa tamaa kwani Mungu hufanya mambo yake kwa wakati ufaao.
Kulingana na ushuhuda wa pasta huyo, yeye na mkewe walikuwa wakimuomba Mungu kila siku kwamba aweze kuwabariki na mtoto hata iwe katika miaka ya uzeeni.
Read ENGLISH VERSION
Je, unayo taarifa inayoweza kubadilisha maisha ya mtu na ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia news@tuko.co.ke; obed.simiyu@tuko.co.ke au WhatsApp: 0732482690 na Telegram: Tuko news.
Tazama habari zaidi kutoka TUKO TV
Subscribe to watch new videosChanzo: TUKO.co.ke
ncG1vNJzZmijmajEorTIpaBnrKWgvG%2BvzmeinmdiboZ2gI9mqqGZnpzEpnnBmpidmV2urm65yp5ksJldorW2rsiroGajpaWuta2MpquorJ9iuqqtyppka2pdqa6vs9Rmoq6nnJrEonrHraSl